MigogoroUlaya
Nchi za Ulaya zazindua mkutano wa kusaidia ujenzi wa Ukraine
11 Julai 2025Matangazo
Waziri Mkuu wa Italia Giorgia Meloni na rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky waliufungua mkutano huo kwa kuwatolewa wito wamiliki wa makampuni na watu binafsi kuwekeza katika miradi itakayosaidia mpango huo.
Mkutano huo umefanyika wakati Urusi ikizidisha mashambulizi nchini Ukraine kwa usiku wa pili mfululizo huku Umoja wa Mataifa ukitahadharisha kuwa idadi ya wahanga wa mashambulizi hayo imefikia kiwango cha juu zaidi.
Hayo yakiarifiwa, rais wa Marekani Donald Trump amesema bila kutoa maelezo zaidi kwamba siku ya Jumatatu atatoa "taarifa muhimu" kuhusu Urusi.