Viongozi wa Ulaya kukutana Paris kuijadili Ukraine
2 Septemba 2025Matangazo
Viongozi kadhaa wa Ulaya akiwemo pia rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky watakutana Alhamisi mjini Paris, huku wengine karibu 30 wakishiriki kwa njia ya mtandao katika mazungumzo ya kujadili suala la hakikisho la usalama kwa Ukraine baada ya vita.
Hayo yakiarifiwa, Moscow na Kiev zimeendelea kushambuliana vikali ambapo watu wawili wameripotiwa kuuawa mjini Kiev na katika mkoa wa Zaporizhzhya huku shambulizi ya Ukraine katika mji mkuu wa mkoa wa Rostov nchini Urusi, likisababisha watu zaidi ya 300 kuhamishwa katika makazi yao.