Viongozi wa Ulaya kujumuika na Zelenskyy mkutano na Trump
18 Agosti 2025Matangazo
Mkutano huo unafuatia mazungumzo kati ya Trump na Rais Vladimir Putin wa Urusi yaliyofanyika Ijumaa iliyopita kama sehemu ya juhudi za hivi karibuni kabisa za kumaliza uvamizi wa Urusi nchini Ukraine.
Viongozi watakaoambatana na Zelenskyy mjini Washington ni pamoja na Rais wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya, Ursula von der Leyen, Kansela Friedrich Merz wa Ujerumani, Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa, Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer na yule wa Italia Giorgia Meloni.
Ajenda kuu itakuwa ni kujadili mapendekezo ya kumaliza vita yanayojumuisha Ukraine kuachia baadhi ya maeneo ya ardhi yake kwa Urusi kwa ahadi ya kupatiwa hakikisho la usalama kwa siku za usoni.