Viongozi wa jumuiya ya SADC kujadili mgogoro wa Kongo
13 Machi 2025Matangazo
Mkutano huo wa kilele pia utatathmini muda wa kuendelea kubakia kwa kikosi chake cha kilichoko kwenye eneo hilo tete ambacho kimeshapoteza wanajeshi wake 17 mwaka huu kufuatia mapigano na waasi wa M23.
Soma pia:Mkutano wa pamoja wa EAC, SADC wamalizika Dar es Salaam
Mkutano huo utafanyika baada ya hapo jana Jumatano, Angola ambayo ni msuluhishi kwenye mgogoro huo,kutangaza kwamba serikali ya Kongo na waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda watafanya mazungumzo ya amani wiki ijayo nchini Angola.Taarifa hiyo ilitangazwa na ofisi ya rais Joao Lourenco.