China na Thailand zaapa kupambana na utapeli wa mitandaoni
6 Februari 2025Matangazo
Viongozi hao wawili wameyasema hayo wakati walipokutana mjini Beijing.
Myanmar, Cambodia na Laos, ambazo ziko kusini mwa China na zinapakana na Thailand, zimekuwa vituo vikuu vya shughuli za utapeli wa mitandaoni ambapo watu wanaoshawishiwa na matangazo ya uwongo ya kazi zinazolipa vizuri husafirishwa hadi kwenye maeneo ya faragha
Na baadae hulazimishwa kufanya kazi na vikundi vya uhalifu vinavyoendesha utapeli mtandaoni unaolenga watu kote ulimwengu.
Maafisa wa Tahiland na China wamechukua hatua za wazi kulishughulikia sakata hilo la utapeli, ikiwemo ziara ya eneo la mpakani ya Liu Zhonyi, naibu waziri wa usalama wa umma wa China.