SiasaAsia
Vikosi vya India na Pakistan vyashambuliana Kashmir
25 Aprili 2025Matangazo
Maafisa wawili wa ujasusi, wameliambia shirika la habari la dpa kwamba vikosi vya India vilifanya mashambulizi ya risasi ya usiku kucha katika kituo cha mpakani katika eneo la Leepa nchini Pakistan.
Mzozo wazidi kufukuta kati ya India na Pakistan baada ya shambulio Kashmir
Afisa mmoja ameongeza kuwa vikosi vyao vilijibu shambulizi hilo kwa silaha nyepesi lakini mashambulizi hayo yamesitishwa kwa sasa na hakuna majeruhi walioripotiwa.
Pakistan yazifungia ndege za India anga yake
Mashambulizi hayo yanakuja baada ya mataifa hayo mawili ya Asia Kusini kulumbana mapema wiki hii baada ya shambulizi baya la kigaidi katika eneo hilo la Kashmir linalotawaliwa na India lililosababisha vifo vya watalii 26.