JamiiVatican
Vatican: Makadinali wawili hawatashiriki kumchagua Papa mpya
29 Aprili 2025Matangazo
Vatican haikutaja majina ya makadinali hao lakini chanzo kutoka jimbo kuu la Valencia kiliithibitishia AFP kwamba askofu mkuu mstaafu, Kadinali Antonio Canizares, hatahudhuria mkutano huo kutokana na sababu za kiafya.
Vatican yasema Mkutano Maalumu wa kumchagua Papa mpya kuanza Mei 7
Jumla ya makadinali 135 wanastahili kupiga kura katika hafla hiyo ya siri itakayofanyika katika eneo dogo la ibada la Sistine itakayoanza Mei 7 na kutarajiwa kudumu kwa siku kadhaa.
Mrithi wa Papa Francis anahitaji thuluthi mbili ya kura
Ikiwa makadinali wengine wote watahudhuria, kutakuwa na makadinali 133 watakaoshiriki kura hiyo.
Mshindi atakayemrithi Papa Francis atahitaji angalau thuluthi mbili ya kura, idadi ambayo sasa imefikia 89.