MigogoroUlaya
Urusi: Marekani na Ulaya ziache kuipatia Ukraine silaha
10 Mei 2025Matangazo
Moscow iliitupia pia lawama Ukraine kwamba inayakwepa mazungumzo ya kina ya kuumaliza mzozo kati yao.
Hayo yameelezwa Jumamosi na Msemaji wa Ikulu ya Kremlin Dmitry Peskov akisisitiza kuwa, ikiwa makubaliano hayo yatafikiwa bila ya sharti hilo kutekelezwa, itakuwa ni faida kubwa kwa Ukraine ambayo itatumia muda huo kujipanga upya kijeshi na kusogeza vikosi zaidi maeneo ya karibu na mpaka.
Kauli hiyo imetolewa siku moja baada ya Urusi kufanya gwaride kubwa la kijeshi ili kusherehekea "Siku ya Ushindi" dhidi ya utawala wa manazi wa Ujerumani ambayo inaadhimisha pia miaka 80 tangu kumalizika kwa Vita Vya Pili Vya Dunia.