MigogoroUlaya
Urusi: Tumekiteka kijiji kingine Ukraine
13 Julai 2025Matangazo
Wizara ya Ulinzi ya Urusi imekitaja kijiji hicho kuwa ni cha Myrne kilicho karibu na mpaka kati ya mikoa hiyo. Wakati Moscow ikitangaza mafanikio hayo, Shirika la Ujasusi la Ukraine limearifu kuwa limewauwa watu wawili wanaoshukiwa kuwa walimuuwa jasusi wa Ukraine mjini Kyiv Alhamisi wiki hii.
Mkuu wa Shirika la Ujasusi la Ukraine Vasyl Malyuk, amesema watu hao, mwanamke na mwanaume waliokuwa mafichoni wakati wa operesheni maalumu waligoma kujisalimisha na walianzisha mapambano ya risasi ambapo hatimaye waliuawa.