Urusi yasema imedungua droni 8 zilizorushwa kutokea Ukraine
7 Julai 2025Matangazo
Wizara hiyo imesema droni nyingi zilizodunguliwa zilianguka katika maeneo yaliyoko karibu na Ukraine na droni tatu ziliharibiwa katika eneo la Leningrad lililo karibu na mji wa pili kwa ukubwa nchini Urusi wa St Petersburg.
Kwa kawaida wizara ya ulinzi nchini Urusi huwa inaripoti tu kuhusu idadi ya droni zilizodunguliwa na hairipoti kuhusu hasara iliyotokea.
Putin aionya Ujerumani kuipatia Ukraine makombora ya Taurus
Hata hivyo magavana wa maeneo yaliyoshambuliwa wamesema uharibifu wa majengo haukuwa mkubwa.
Mamlaka ya udhibiti wa anga ya Urusi imeripoti kufungwa kwa viwanja vya ndege katika miji miwili baada ya mashambulizi hayo yaliyosababisha pia kucheleweshwa kwa safari za ndege.