Urusi yapongeza Ukraine kuwa tayari kwa mazungumzo ya amani
5 Machi 2025Matangazo
Kauli ya Zelensky ilitolewa katika barua iliyotumwa kwa Rais wa Marekani Donald Trump na kuwekwa hadharani jana, kauli iliyoainisha pia kuwa Kiev itasaini makubaliano ya madini na Marekani.
Ikulu ya Ufaransa ya Elysée imesema rais Emmanuel Macron anatarajiwa kurejea mjini Washington kukutana na Trump akiambatana na Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer na rais Zelensky.
Zelensky asema muafaka wa amani na Uusi unawezekana ikiwa Moscow itakubali masharti
Macron atalihutubia Bunge huku viongozi wa Ulaya wakikutana kesho katika mkutano wao wa kilele utakaojadili masuala ya ulinzi na mzozo wa Ukraine.