MigogoroUlaya
Kremlin: Urusi haitorefusha muda wa usitishwaji mapigano
30 Aprili 2025Matangazo
Hatua ya Putin inatarajiwa kuanza kutekelezwa Mei 8 hadi 11, ili kuadhimisha mwisho wa Vita vya Pili vya Dunia. Hata hivyo Msemaji wa Ikulu ya Kremlin Dmitry Peskov amesema wamelipokea pendekezo hilo lililotolewa na rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky lakini akasema haliwezekani kabla ya masuala kadhaa kupatiwa ufumbuzi.
Hayo yanajiri wakati miito mbalimbali imetolewa kwa Urusi kusitisha mashambulizi na kufikia makubaliano ya kuvimaliza vita hivyo, huku Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio akitishia kuwa nchi yake itajiondoa kama mpatanishi kwenye mzozo huo ikiwa hakutokuwa maendeleo yoyote yatakayoshuhudiwa.