Urusi yakataa kupelekwa kwa vikosi vya Ulaya nchini Ukraine
27 Agosti 2025Matangazo
Msemaji wa ikulu ya Kremlin Dmitry Peskov, amesema wana mtazamo mbaya kuhusu mijadala ya uwezekano wa kikosi cha kulinda amani cha Ulaya kama sehemu ya makubaliano ya kumaliza vita vya Urusi nchini Ukraine.
Peskov amesema haya wakati wa mkutano na waandishi wa habari.
Trump na Putin wamemaliza mkutano bila makubaliano kuhusu vita vya Ukraine
Peskov amesema mwanzoni kabisa ilikuwa ni kupelekwa kwa vifaa vya kijeshi vya NATO ndani ya Ukraine kunakoweza kutajwa kuwa miongoni mwa sababu ya msingi za mgogoro uliotokea
Msemaji huyo wa Kremlin pia amesema wakuu wa timu za mazungumzo zaUrusi na Ukraine wanawasiliana lakini hakuna tarehe iliyowekwa kwa mazungumzo ya baadaye.